MSANII mkali wa kuchekesha na sanaa za jukwaani Afrika Mashariki, Anne
Kansiime anatarajiwa kufanya onyesho lake Agosti 2, mwaka huu katika
Ukumbi wa Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo linaloandaliwa na kituo cha Redio 5 litaambatana na burudani
ya muziki kutoka kwa Odama Band, pamoja na mchekeshaji Fredi Omondi
kutoka Kenya na Pilipili wa Tanzania.
Akizungumzia onyesho hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Redio 5,
Robert Francis alisema wameamua kumualika Kansiime kwa sababu ana kipaji
cha hali ya juu katika uchekeshaji na ana mashabiki wengi Tanzania.
“Kansiime ni mchekeshaji ambaye amejizolea umaarufu mkubwa Afrika
Mashariki kwa uwezo wake wa kuweka utani kwenye maisha ya kawaida,”
alisema Francis.
Cheki Moja ya Comedy Zake Hapo chini
Kansiime maarufu katika mitandao ya kijamii, alianza kwa kuweka vipande
vya video akiigiza kama mwanamke wa Kiafrika anayekutana na changamoto
mbalimbali za maisha.
Pia, huendesha kipindi cha ‘Don’t Mess With Kansiime’ kwenye kituo cha
Citizen TV, anatajwa kuwa mwanamke mwenye kipaji cha pekee nchini Uganda
na Afrika Mashariki kwa ujumla. Onyesho hilo la Kansiime, limepewa jina
la Cheka Kwa Nguvu, na tiketi zitauzwa Sh.90,000 kwa mtu mmoja na
Sh.700,000 kwa meza ya watu wanane.
0 comments :
Post a Comment