Al-Shabaab imekuwa ilkilazimisha kutorosha watoto kutoka katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao kwa kisingizio kwamba wanatoa malazi na elimu kwa vijana wasio na makaazi na wasiotunzwa, wazazi wanaohusika na wazee waliiambia Sabahi.
  • Picha iliyotumwa katika tovuti ya Redio Al-Furqaan ikionyesha watoto wakiwa wamekaa katika kituo kinachodaiwa kuwa ni kwa ajili ya vijana walio katika mazingira hatarishi ambacho kilifunguliwa na al-Shabaab huko Barawe tarehe 29 Juni. [File] www.bongohots.blogspot.com Picha iliyotumwa katika tovuti ya Redio Al-Furqaan ikionyesha watoto wakiwa wamekaa katika kituo kinachodaiwa kuwa ni kwa ajili ya vijana walio katika mazingira hatarishi ambacho kilifunguliwa na al-Shabaab huko Barawe tarehe 29 Juni. [File]
Lengo la kituo hiki ni kurekebisha watoto "wasiotunzwa" na kuwapa elimu ya dini, kiongozi wa al-Shabaab katika Shabelle ya Chini Sheikh Mohamed Abu Abdalla alisema katika ujumbe wa sauti uliotumwa katika tovuti ya Redio Al-Furqaan, msemaji kwa niaba ya kikundi.
"Ni kituo cha kurekebisha watoto ambao wamepotoka au wasio na makaazi na ambao wameachwa bila kutunzwa na umma," Abdalla alisema katika uzinduzi.
Zaidi ya mayatima, alisema, kituo kitawapokea watoto wengine ambao wanahitaji kurekebishwa na kutoa wito kwa wazazi wa watoto walioacha shule na familia zinazorejea Somalia kutoka nje ya nchi kuandikisha watoto wao.
"Watoto waliorudi Mogadishu wakitokea nchi za Magharibi wanahitaji urekebishaji," alisema. "Ninatoa wito kwa watu waliotawanyika duniani wakitokea Somalia kutumia fursa hii [ya kituo hiki]."
Lakini licha ya kuhudumia watoto mayatima na walio katika mazingira hatarishi, kituo hiki kimejazwa watoto waliochukuliwa majumbani kwao na shuleni, alisema Sultan Ali Hassan Ibrahim, mzee mwenye umri wa miaka 60-kutoka Barawe ambaye alikimbilia Mogadishu mnamo Novemba 2013 kutokana na wasiwasi juu ya usalama wake.
"Watu [wa Barawe] hawako huru, kwa hiyo watoto wao wanawekwa katika makambi yanayoitwa ya urekebishaji pasipo ridhaa yao," aliiambia Sabahi. "Wamewaweka vijana wadogo katika makambi, hususani watoto wa kati ya umri wa miaka 12 na 16, ambao wanaamini wanaweza kuwatia kasumba kwa haraka kuamini kile wanachoridhishwa."
Ibrahim alisema al-Shabaab imefungua makambi yanayofanana na hayo ya kutia kasumba huko Sablale katika Shabelle ya chini, na huko Buale, mji mkuu wa Jubba ya kati.
Alisema watoto sita ambao alikuwa na uhusiano nao ni miongoni mwa hao waliotoroshwa na al-Shabaab.
"Hawatenganishi watoto. Hata hivyo wamekuwa wakiwachukua wale wanaokwenda shule na wale wanaojifunza katika misikiti," alisema. "Watoto hawaruhusiwi kutembelewa na ndugu zao."

Hila za kuongeza tena wapiganaji wa al-Shabaab

Pamoja na madai ya al-Shabaab, lengo la kundi la wanamgambo ni kuongeza tena vyeo vya wapiganaji ambavyo walipoteza katika mapigano, alisema Mohamed Yaqub, mwenye umri wa miaka 38, ambaye alikimbia kutoka Barawe pamoja na mke wake na watoto wakati al-Shabaab walipoteka eneo hilo.
"Wanataka kuwaingiza katika jeshi watoto na kuwatumika katika mapigano," alisema. "Kusudi lao sio kuwahudumia [kama walivyodai]."
Abukar Sheikh Hassan, mzee wa mila mwenye umri wa miaka 55 ambaye pia alikimbia kutoka Barawe miaka miwili iliyopita ambaye sasa anaishi Mogadishu, aliiambia Sabahi kwamba wananchi wa Barawe wana wasiwasi wa siku zijazo za watoto wao.
"Kusudi la al-Shabaab sio kuwafundisha watoto Qur'an na dini, bali wanataka watoto kujilipua wenyewe," aliiambia Sabahi.
Hassan alionyesha wasiwasi wake kwamba watoto wanaweza kurejea nyumbani kuua familia zao na wananchi wenzao wa Barawe ambao walibadilishwa mawazo na mtazamo uliobadilika na vurugu za al-Shabaab.
"Watu ambao wangekuwa sehemu katika maendeleo ya mkoa kwa kupata elimu nzuri na kuusaidia umma wanakuwa watu ambao wanapita njia isiyofaa," alisema.
Kutangaza kufunguliwa kwa Kituo cha al-Amal, al-Shabaab walituma picha za watoto waliovaa sare safi na wakiwa wameshikilia nakala za Qur'an, wakidai kwamba maisha ya watoto hao yamekuwa bora zaidi.
Lakini Hassan alisema kwamba ni propaganda tu ambazo al-Shabaab wanatumia kuwatega watoto na kuwashawishi wazazi kuja katika maeneo yaliyopo chini ya udhibiti wa al-Shabaab kwa ajili ya kutafuta maisha mazuri.
Badala yake, alisema serikali ya Somalia inapaswa kutoa huduma za kuboresha maisha ya watoto wasiokuwa na makazi na yatima ambao hawana mtu kuwatunza.
"Serikali inapaswa kukamilisha wajibu wake na kuonyesha utawala bora na kuwatunza watoto," alisema. "Vinginevyo al-Shabaab watachukua wajibu huo na kuwabadilisha mawazo watoto.

0 comments :

Post a Comment

 
Top
Bongohots.blospot.Com