Gotze, aliefunga bao la ushindi dhidi ya Argentina wakati wa mchezo wa hatua ya fainali kwenye michuano ya kombe la dunia ameonekana katika hali hiyo akiwa na rafiki yake wa kike, Ann Kathrin Brömmel.
Wawili hao walikutwa wakiogelea kwenye dimbwi la matope katika moja ya fukwe huko nchini Ujerumani, na kisha walijitokeza hadarani wakiwa na mandhari ya kama watu waliorukwa akili, lakini mwisho wa siku imefahamika ilikuwa ni moja ya starehe yao wakiwa mapumzikoni.
Ann Kathrin, kwa mara ya mwisho alionekana akiwa na Mario Gotze mara baada ya mchezo wa hatua ya fainali wa michuano ya kombe la dunia dhidi ya Argentina, uliochezwa nchini Brazil katika uwanja wa Maracana, akishangilia ushindi wa bao moja kwa sifuri.




0 comments :
Post a Comment