![]() |
Shambulizi
hilo lilisababisha vifo vya wapalestina 128 na kusababisha zaidi ya mamilion ya watu kukosa
umeme baada ya mitambo ya umeme kuharibiwa vibaya katika mashambulizi hayo
yaliyofanywa siku ya jumanne.
Kwa
mujibu wa afisa wa afya wa Palestina Ashraf al Kidra alipozungumza na Associated
Press alisema vifo vya jana vinatimiza idadi ya wapelestina waliokufa kutokana
na vita hivyo kufikia 1,229 huku zaidi ya 7,000 wakibaki na majeraha, ilihali serikali
ya Israel ilisema imepoteza uhai wa wanajeshi wake 53.
Pamoja
na madhara yanayoendelea kutokea baina ya nchi hizo mbili, pande zote mbili
zinasisitiza kutositisha mashambulizi.
Kiongozi
wa Hamas alisema hawatasitisha mashambulizi ya roketi mpaka pale
watakapotimiziwa matakwa yao, huku waziri mkuu wa Israel naye akiwaonya
waisrael kujiandaa kwa vita zaidi
Hata
hivyo jitihada za kimataifa zinazoongozwa na Misri zinaendelea ili kusitisha
mapigano hayo kwasababu za kubinadamu.
0 comments :
Post a Comment